Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) ameielekeza menejimenti ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kubuni mikakati ya kuongeza mapato yatokanayo na Utalii ikiwa ni maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Waziri Chana ametoa kauli hiyo leo
Oktoba 16,2024 alipokuwa akizungumza na Menejimenti ya Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro katika Ofisi zao zilizopo jijini Arusha.
"Niwapongeze kwa kazi nzuri
mnayoifanya lakini Mheshimiwa Rais anataka tuongeze mapato na tubuni mazao mapya ya utalii, " amesisitiza.
Aidha, ameielekeza Taasisi ya Utafiti
wa Misitu Tanzania (TAFORI) ihakikishe inatoa ufumbuzi wa changamoto ya magugu
vamizi yanayoharibu uoto wa asili ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro.
"Natoa siku saba kwa TAFORI
waende katika bonde la Kreta na kutoa
ufumbuzi wa namna ya kudhibiti mimea vamizi," amesisitiza Mhe. Chana.
Naye, Naibu Katibu Mkuu
anayeshughulikia Utalii, Nkoba Mabula ameitaka mamlaka hiyo kuwa wabunifu,
kuangalia namna ya kujitangaza na kubuni mazao mengine ya utalii ili kuiongezea
Serikali mapato.
0 Maoni