Milioni 2.3 hubainika kuwa na Saratani ya matiti kila mwaka

 

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema kila mwaka kuna wagonjwa wapya milioni 2.3 wa Saratani ya matiti wanaogundulika duniani.

WHO imetoa taarifa yake hiyo katika mwezi huu wa Oktoba ambao hutumika katika kuwaelimisha watu duniani kuhusiana na Saratani.

Taarifa hiyo ya WHO imesema nusu ya wanawake wanaougua Saratani huwa hawana dalili za kuwa katika hatari za kuugua ugonjwa huo, bali ni kwa kuwa ni wanawake ama kuzeeka.

Kupunguza vifo vya Saratani na matiti kwa asilimia 2.5 kwa mwaka kunaweza kudhibiti asilimia 25 ya vifo ifikapo 2030 na asilimia 40 ifikapo mwaka 2040 kwa wanawake wenye umri wa zaidi ya miaka 70.

Saratani ya matiti ni ugonjwa unaosababishwa na seli zisizozakawaida zinazokua na kushindwa kudhibitiwa na kisha kugeuka kuwa uvimbe kwenye matiti.

Iwapo mtu anayeugua Saratani ya matiti asipofanyiwa uchunguzi uvimbe huo utasambaa mwilini na kuhatarisha maisha.

Chapisha Maoni

0 Maoni