Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu ameipongeza Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kwa shughuli za utafiti wa Wanyamapori ambazo zina tija katika sekta ya uhifadhi na utalii ambayo inachangia asilimia 17% ya pato la Taifa.
Akizungumza jana Oktoba 21, 2024
wakati wa kikao na Menejimenti ya TAWIRI, Bw. Mchechu amesema Ofisi ya msajili
wa Hazina itaendelea kushauri vyema katika kuimarisha Mashirika ya Umma yaweze
kujiendesha kwa tija.
“Nawapongeza kwa utendaji mzuri, nitoe
wito kuendelea kuwa wabunifu kutumia rasimali mlizo nazo kujiendesha kwa
ufanisi,” amehimiza Bw. Mchechu.
Naye, Mkurugenzi Mkuu TAWIRI Dkt,
Eblate Mjingo amesema TAWIRI ni taasisi ya kimkakati ambayo mbali na kutokuonekana ikizalisha
fedha moja kwa moja ina mchango
mkubwa katika mapato yatokanayo na utalii nchini ambapo takwimu na
taarifa za tafiti ndizo zinazonadi utalii na kuimarisha uhifadhi.
0 Maoni