Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da
Silva amesitisha safari yake ya kwenda Urusi baada ya kuumia kichwani katika
ajali iliyotokea nyumbani siku ya Jumamosi.
Lula mwenye umri wa miaka 78, alikuwa
asafiri sku ya jumapili alasiri kushiriki mkutano wa Jumuiya ya Nchi
Zinazoendelea za Brazil, Urusi, India, China na Afrika Kusini (BRICS)
Hospitali Kuu ya ya Mji wa Brasilia
imemshauri Rais Lula, kujiepusha na safari ndefu za ndege kwa muda.
Kutokana na hali hiyo Lula sasa
itabidi ashiriki mkutano huo wa BRICS kwa njia ya mdandanoni ya mkutano kwa
njia ya video.
0 Maoni