Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga
Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) akiwa na mwenyeji wake Mkuu wa
Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu akipokea kikosi maalumu cha Jeshi la Wananchi
wa Tanzania (JWTZ) kilichopandisha Mwenge wa Uhuru na Bendera ya Taifa katika
kilele cha Mlima Kilimanjaro leo tarehe 21-10-2024 katika Lango la Marangu
linalotumika kwa ajili ya kupandia na kushukia watalii lililopo Mkoani
Kilimanjaro.
Mapokezi ya awali ya Kikosi hicho
yaliongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Jacob Mkunda.
0 Maoni