Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania
Jenerali Jacob Mkunda, tayari amewasili katika Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro
tayari kwa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru kutoka kilele cha Mlima Kilimanjaro.
Jenerali Mkunda amepokelewa leo tarehe
21, Oktoba 2024 na mwenyeji wake Kamishna wa Uhifadhi TANAPA, Musa Nassoro Kuji.
Ikumbukwe kuwa tarehe 14, Oktoba 2024
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi la Ulinzi na Usalama Rais Samia Suluhu Hassan
alimkabidhi Mwenge wa Uhuru na Bendera Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob
Mkunda, ili Jeshi hilo liupeleke kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro ikiwa ni
sehemu ya sherehe za miaka 60 tangu kuanzishwa kwa mbio za mwenge huo.
Ambapo tarehe 15, Oktoba 2024 Kikosi
maalumu cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kilianza safari ya kupandisha
Mwenge wa Uhuru na Bendera ya Taifa katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.
0 Maoni