MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) na Mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa mwishoni mwa wiki hii,
ameshuhudia madiwani wawili na Katibu Kata kutoka vyama vya CUF na
ACT-Wazalendo wakirejea CCM.
Akiwa kwenye kijiji cha Milola katika siku
ya kwanza ya ziara yake, Mheshimiwa Majaliwa alishuhudia madiwani wa Kata za
Milola na Rutamba wakitambulishwa na Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Mama Salma
Kikwete katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye senta ya Milola, Kata ya
Milola, Manispaa ya Lindi.
Viongozi waliorejea CCM ni Diwani wa
Milola, Bw. Hussein Kimbyoko kutoka Chama cha Wananchi (CUF) na Diwani wa
Rutambi, Bw. Athumani Mmaije kutoka Chama cha ACT – Wazalendo.
Akiwa katika siku ya pili ya ziara
yake jimboni Ruangwa, Mheshimiwa Majaliwa alishuhudia wanachama wengine wawili
wakikabidhi kadi zao kwa Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Ruangwa, Mzee Ibrahim
Issa Ndoro katika mkutano uliofanyika kwenye viwanja vya Wandorwa, wilayani
Ruangwa, mkoani Lindi.
Wanachama hao ni Alhaji Abasi Abdallah
Chinguwile kutoka ACT WAZALENDO ambaye alikuwa mwanachama katika kijiji cha
Mmawa, Kata ya Likunja, wilaya ya Ruangwa. Mwingine ni Bw. Jafari Juma
Nang’anda kutoka CUF ambaye pia alikuwa ni Mkurugenzi wa Uchaguzi na Katibu
Kata wa Kata ya Nachingwea, wilayani humo.
Akizungumza baada ya kupokewa na
viongozi wa CCM, Bw. Jafari Nang’anda alisema ana imani na viongozi wa CCM wa
mkoa na wilaya na akawaomba watambue kuwa anaweza kufanya kazi saa yoyote na
mahali popote.
0 Maoni