Naibu Rais wa Kenya aliyeondolewa
wadhifa wake na Baraza la Seneti la Kenya, Rigathi Gachagua, ametoka hospitali leo
na kulalamika kuondolewa walinzi wake akiwa amelazwa hospitali.
Gachagua akiongea nje ya hospitali
aliyolazwa amesema,"Nibahati mbaya wakati nikiwa hapa hospitali, kaka
yangu na rafiki yangu Rais William Ruto ameagiza niondolewe ulinzi."
Amesema kwamba licha ya yeye
kuondolewa ulinzi hospitali, pia walinzi waliokuwa nyumbani yake ya Karen Jijini
Nairobi na nyumba ya kwao Nyeri pia wameondolewa.
Kama hiyo haitoshi, Gachagua amedai kuwa watumishi wote waliokuwa kwenye Ofisi Naibu Rais wamepewa likizo ya dharura na
magari yote yaserikali yamechukuliwa.
Gachagua amesema anashangaa kufanyiwa
hayo yote na Rais William Ruto wakati akijua kwamba Mahakama imetoa zuio la uamuzi
wa kuenguliwa kwake madarakani na Baraza la Seneti.
0 Maoni