Mafuriko yaua watu wapatao 95 Hispania

 

Waokoaji kusini mwa Hispania wanafanyakazi bila ya kuchoka kutafuta iwapo bado kuna mtu yeyote aliyepotea baada ya mafuriko yaliyoua watu wapatao 95.

Haijafahamika hadi sasa idadi ya watu ambao hawajapatikana, lakini mamia ya wanajeshi wamepelekwa huko Valencia kusaidia, eneo moja wapo lililoathirika mno.

Baadhi ya maeneo yanaweza kufikika kwa helkopta tu, kutokana na barabara kujaa matope zito, vifusi na magari yaliyopandiana.




Chapisha Maoni

0 Maoni