Mahakama ya Sheria ya Milimani iliyopo
jijini Nairobi nchini Kenya inaendelea kusikiliza kesi ya kuenguliwa madaraka na
Seneti, Naibu Rais wa Kenya Rigathi Gachagua
Gachagua aliwasili mahakamani akiwa na
wanasiasa wanaomuunga mkono, akiwamo aliyekuwa Katibu Mkuu wa UDA Cleophas
Malala, Gathoni Wamuchomba, Njeri Maina, pamoja na Mbunge wa Embakasi ya Kati Benjamin
Gathiri, na wengineo.
Kesi hizo mbili, moja yakupinga
kuenguliwa Gachagua, na nyingine kuapishwa kwa mrithi wake, zinasikilizwa na jopo
la majaji Fredah Mugambi, Eric Ogola pamoja na Anthony Mrima.
Katika kesi hizo upande wa Gachagua
unawakiliswa na Wakili Mwandamizi Paul Muite, akishirkiana na Elisha Ongoya,
Ndegwa Njiru, pamoja na mawakili wengine.
0 Maoni