Waziri Mkuu
Kassim Majaliwa ameshiriki katika
ufunguzi wa Mkutano wa ngazi ya juu wa Wakuu wa Nchi na Serikali ‘Summit of the
Future’ uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Umoja wa Mataifa New York
nchini Marekani.
Mkutano huo uliofanyika
jana unawaleta pamoja viongozi wa nchi na Serikali duniani ili kujadili masuala
mbalimbali ya maendeleo na namna wanaweza kuboresha hali ya sasa na kuzilinda
siku zijazo.
Mheshimiwa
Majaliwa yupo nchini Marekani kumwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika
mkutano Mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA79).
0 Maoni