Wauzaji dhahabu nje watakiwa kuiuzia BoT asilimia 20 ya dhahabu

 

Kuanzia Oktoba mosi mwaka huu, mchimbaji ama mfanyabiashara wa dhahabu anayetaka kusafirisha dhahabu nje ya nchi, anapaswa kutenga asilimia 20 ya dhahabu yote anayotaka kusafirisha nje, kwa ajili ya kuiuzia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu Mtendaji Tume ya Madini Mhandisi Ramadhani Lwamo imesema kiasi hicho cha asilimi 20 ya dhahabu kinapaswa kuwasilishwa katika viwanda vya kusafisha dhahabu (refineries) vya Eyes of Africa Ltd cha Dodoma na Mwanza Precious Metals Refineary Ltd cha Mwanza.

Taarifa hiyo imesema kwamba taratibu za malipo ya dhahabu hiyo ya kiwango cha asilimia 20 ya dhahabu itakayouzwa nje, zitafanywa kwa mujibu wa Benki Kuu ya Tanzania. Takwa hili ni kwa mujinu wa kifungu cha 59 cha Sheria ya Madini, Sura ya 123.

Utaratibu huu unakuja kufuatia kupitishwa kwa Muswada wa Fedha wa Mwaka 2024/2025 na Bunge la Jamhuri ya Muungani wa Tanzania, ambapo Sheria ya Madini inamtaka kila mchimbaji ama mfanyabishara wa madini kutenga asilimia 20 ya dhahabu inayozalishwa kwa ajili ya kuiuzia BoT, kabla ya kuisafirisha nje ya nchi.

Chapisha Maoni

0 Maoni