TAWA yashiriki Kongamano la Siku ya Utalii Duniani

 

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) imeshiriki katika maonesho na  kongamano la maadhimisho ya siku ya utalii duniani lililoanza tarehe 26/9/2024 na kufikia kilele 27/9/2024 katika hoteli ya Gran Melia jijini Arusha.

TAWA ikiwa ni sehemu ya wadhamini  wa kongamano hilo,  imetumia nafasi hii kukutana na wadau mbalimbali wa tasnia ya utalii  kuelezea vivutio adhimu ilivyonavyo katika maeneo inayosimamia pamoja na  fursa za uwekezaji katika maeneo hayo.

Mgeni rasmi katika kongamano hilo alikuwa ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Dastan Kitandula (Mb) aliyepongeza jitihada zinazofanywa na sekta binafsi katika kuuza vivutio vya nchi yetu, alisisitiza mchango wa utalii katika uchumi wa nchi yetu na kuelezea ni namna gani Serikali inaboresha miundombinu ya utalii pamoja na kufungua soko la utalii kwa upande wa kusini mwa Tanzania.

Kongamano hili limeandaliwa na Chuo Cha Uhasibu Arusha kwa kushirikiana na taasisi ya Rethinking Tourism Africa likiwakutanisha  wadau wa sekta ya utalii kutoka ndani na nje ya Tanzania.



Chapisha Maoni

0 Maoni