Profesa Mkorea aipongeza Mloganzila kwa kuendelea kuboresha huduma

 

Daktari Bingwa Mbobezi wa Upasuaji Ubongo Mgongo na Mishipa ya Fahamu Prof. Huh Seung Kon kutoka Korea Kusini ameupongeza uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kwa mageuzi na maboresho makubwa iliyofanya katika kuendelea kuberesha utoaji wa huduma za afya nchini.

Prof. Huh ametoa pongezi hizo alipotembelea hospitali hiyo kwa lengo la kukutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa hospitali pamoja wataalam wanaofanya kazi katika Idara ya Upasuaji Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu idara ambayo amehuduma kwa kipindi cha takribani miaka minne kabla ya kurejea nchini Korea mwaka 2022.

Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi Mtendaji MNH-Mloganzila Dkt. Julieth Magandi amemshukuru Prof. Huh kwa ujio wake kwani unaendelea kuongeza chachu katika kutoa huduma za ubingwa bobezi katika hospitali hiyo kwa manufaa ya Watanzania.

Dkt. Magandi ameongeza kuwa Muhimbili-Mloganzila imeendelea kunufaika na Prof. Huh na kutoa mfano kuwa wauguzi watatu walienda kupata mafunzo ya muda mfupi nchini Korea na wengine watatu wapo nchini Korea kwa mafunzo kwa ufadhili wa daktari huyo.

Prof. Huh alikuja nchini kwa mara ya kwanza mwaka Disemba mwaka 2019 na kuondoka nchini mwaka 2022 ambapo katika kipindi hicho aliwajengea uwezo wataalam wa Idara ya Upasuaji Ubongo Mgongo na Mishipa ya Fahamu  na walifanikiwa kuanzisha huduma ya ubingwa bobezi kwa kutumia njia ya kisasa ya upasuaji wa kuondoa uvimbe kwenye sakafu ya ubongo kwa kutumia matundu ya pua.

Chapisha Maoni

0 Maoni