Mabasi matatu yakamatwa kwa makosa ya barabarani

 

Mkuu wa Oparesheni Kikosi cha Usalama barabarani nchini Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Nassoro Sisiowaya akiwa na wajumbe wa Kamati ya Usalama barabarani Mkoa wa Mbeya alifanya ukaguzi wa kushtukiza kwa madereva wa mabasi ya abiria yanayofanya safari zake kati ya Mbeya kupitia barabara ya Chunya.

Katika ukaguzi huo jumla ya Mabasi ya Abiria 03 yalikamatwa, kukaguliwa na kubainika kuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo mfumo wa breki, ubovu na kuzidisha abiria. Madereva wa vyombo hivyo walichukuliwa hatua mbalimbali ikiwemo kupigwa faini na kurejesha nauli kwa abiria ili kutafutiwa usafiri mwingine.



Chapisha Maoni

0 Maoni