Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimemtangaza Wakili Boniface
Mwambukusi kuwa rais mpya wa chama hicho baada ya kuibuka mshindi katika uchaguzi.
Mwambukuzi amepata ushindi wa kura 1,274 ambazo ni sawa na
asilimia 57.4, huku ikielezwa misimamo na ujasiri wake umechangia kumpatia
ushindi huo.
Uchaguzi huo uliofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kiwete (JKCC) Jijini Dodoma, umefanikiwa kumchagua Mwambukusi kumrithi Harold Sungusia aliyemaliza muda wake.
0 Maoni