Rais Samia ampongeza Eng. Seff kwa kazi nzuri inayofanywa na TARURA

 

Rais Samia Suluhu Hassan amempongeza Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seff kwa kazi nzuri inayofanyika nchini.

Rais Samia ametoa pongezi hizo jana alipozungumza na wananchi wa Berega wilayani Kilosa mara baada ya kufungua daraja la Berega lililojengwa na TARURA.

“Nimpongeze sana sana Mhandisi Seff, wataalam na timu yake ndani ya TARURA kwa kazi nzuri wanayoifanya Tanzania nzima, nimemvisha maua yake,” alisema Rais Samia.

Amesema daraja hilo litasaidia kuwaunganisha wananchi lakini kurahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii.

Pia, Rais Samia amewataka wananchi kutunza daraja hilo, kwa kuwasihi wasichimbe mchanga ili liweze kutumika miaka mingi.

“Wananchi mnaharibu mazingira, fanyeni shughuli zenu kwenye mto lakini msiharibu mazingira msichimbe mchanga kwenye mto huu, daraja hili limechukua fedha nyingi ili wananchi mnufaike, tunzeni daraja hili,” alisema Rais Samia.

Na. Mwandishi Wetu

Chapisha Maoni

0 Maoni