Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia
Suluhu Hassan, amekabidhi cheti cha pongezi kwa Mamlaka ya Usimamizi wa
Wanyamapori Tanzania - TAWA kutokana na ushiriki wake wa kipekee katika Tamasha
la Tisa la Kizimkazi lililofanyika Kusini Unguja, Zanzibar kuazia tarehe 18-25
Agosti, 2024.
Cheti hicho cha pongezi kilipokelewa na Afisa Utalii Mustapha
Buyogera katika hafla ya chakula cha usiku iliyofanyika Ikulu ndogo, Kizimkazi,
Zanzibar.
Katika tamasha hilo, Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia TAWA limekuwa kivutio kikubwa kwa wananchi wengi na wadau mbalimbali wa utalii ambapo wageni walipata fursa ya kushuhudia wanyamapori hai waliopo katika bustani ya wanyamapori hai.
0 Maoni