NSSF itakabidhi Serikali daraja la Kigamboni itaporejesha gharama zake

 

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii ( NSSF), utaendelea kukusanya deni la gharama za la Nyerere Kigamboni hadi hapo utakapo rejesha fedha za mfuko kiasi cha shilingi bilioni 344 ilizotumia hadi kukamilika kwake kwa kipindi cha miaka 30.

Hayo yameelezwa bungeni leo na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akijibu swali la Mbunge wa Kigamboni Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile aliyetaka kujua ni lini NSSF itakamilisha makusanyo ya deni la ujenzi wa Daraja la Nyerere Kigamboni na kulikabidhi Serikalini.

Mhe. Majaliwa amesema mfuko wa NSSF ulianza rasmi uendeshaji wa Daraja la Nyerere Kigamboni mwezi Mei 2016 ambapo hadi kufikia mwezi Julai 2024 sawa na miaka Tisa (9) ya uendeshaji, jumla ya shilingi bilioni 102.18 zimekusanywa kutokana na tozo mbalimbali.

”Fedha kiasi cha shilingi bilioni 344 hizi ni gharama za uwekezaji pamoja na ulinzi na thamani ya fedha iliyowekezwa. Hivyo baada ya fedha hizo kurejeshwa mradi utakabidhiwa Serikalini,” ameeleza Mhe. Majaliwa.

Chapisha Maoni

0 Maoni