Mchezaji wa timu Atletico Awajun amejikuta akitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kuonekana kama anajisaidia haja ndogo nje ya uwanja wakati wa mchezo huko Peru.
Mshambuliaji huyo wa Atletico alinaswa na kamera akionekana
anajisaidia haja ndogo akingojea kupiga mpira wa kona, wakati kipa wa timu
pinzani akiwa anatibiwa.
Licha ya mshambuliaji huyo kuzipa mgongo kamera, akitazama eneo
lisilo na watazamaji, wachezaji wa timu ya Cantorcillo FC walimshtua refa na ndipo
refa akampa kadi nyekundu Munoz.
Maafisa wa Shirikisho la Soka la Peru na wa timu ya Atletico Awajun hawajazungumzia lolote kuhusiana na tuhuma za Munoz.
0 Maoni