Majaliwa aipa kongole Wizara ya Maliasili na Utalii, Maonesho ya Nanenane

 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amefungua Maonesho ya 30 ya Wakulima, Wavuvi na Wafugaji, "Nanenane" amanyo kitaifa yanafanyika Jijini Dodoma na kupongeza Wizara mbalimbali ikiwemo Wizara ya Maliasili na utalii kwa ushiriki kwenye maonesho hayo.

Waziri Mkuu Majaliwa, amesema maonesho hayo yanaumuhimu mkubwa kwa maendeleo ya uchumi wa Taifa na mwananchi mmoja mmoja hivyo ametoa wito kwa wananchi kutembelea maonesho hayo hayo ili kujifunza na kupitia fusra mbalimbali zitakazo wainua kiuchumi. 

Aidha, katika maonesho hayo, Banda la Wizara ya Maliasili limesheheni washiriki mbalimbali zikiwemo taasisi zake pamoja na wadau wake, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanaotembelea banda hilo wanapata hudama stahiki kuhusu Uhifadhi na Utalii.

Pamoja na mambo mengine katika Banda la Maliasili na Utalii, wananchi  watapata fursa ya kujua shughuli za uhifadhi, vivitio vya utalii vilivyopo nchini, kushuhudia vivutio vya utalii mbashara kutoka hifadhi ya Ngorongoro shughuli za  upandaji miti, uanzishaji wa mashamba ya ufugaji wa Wanyamapori,  kuona wanyamapori hai, makumbusho inayotembea,  na shughuli mbalimbali za Wizara ya maliasili na utalii2 pamoja na taasisi zake.

Kauli mbiu ya Maonesho ya nanenane mwaka huu ni "Chagua viongozi bora wa Serikali za mitaa kwa maendeleo endelevu ya Kilimo, mifugo na Utalii.

Chapisha Maoni

0 Maoni