Timu itayoshiriki Michuano ya Olimpiki Paris yakabidhiwa bendera ya taifa

 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Suleiman Selela akimkabidhi tiketi ya ndege nahodha wa timu ya Taifa ya riadha Alphone Felix Simbu katika hafla ya  wachezaji na maofisa wa timu hiyo itakayoshiriki katika  Michezo ya Olimpiki ya Majira ya joto inayoanza  Ijumaa ijayo Julai 26 hadi Jumapili Agosti 11, 2024 jijini Paris na miji mingine 16 nchini Ufaransa

Katika mashindano hayo ya 33 ya Olimpiki, kikosi cha Tanzania kitakuwa na nahodha na mkimbiaji Alphonce Felix Simbu, pamoja na mkimbiaji mwenzie Gabriel Geay ambao watashiriki katika mbio za Marathon kwa wanaume. 

Wengine katika msfara huo ni Jackline Juma Sakilu na Magdalena Crispin Shauri,  ambao watashiriki michuano ya Marathon kwa wanawake. 

Kikosi hicho pia kina waogeleaji wawili, Sophia Anisa Latiff atakayechuana mita 50 freestyle, kategoria ya wanawake na Collins Phillip Saliboko atakayecheza mita 100 freestyle kwa wanaume. 

Mwanamichezo Andrew Thomas Mlugu, atayeshiriki katika mashindano ya mchezo  wa Judo, tayari yuko Paris akiwa katika kambi maalumu ya mchezo huo. 

Timu hiyo itaambatana na makocha watatu wa fani hizo tatu za michezo, daktari wa timu, Mwambata wa  Habari pamoja na maafisa wawili kutoka TOC. 

Zaidi ya wanamichezo 10,500 kutoka mataifa 206 wanatarajiwa kushiriki katika matukio 329 na fani 45 tofauti za michezo. Kwa mara ya kwanza kila jinsia itawakilishwa na wanamichezo 5,250.

Chapisha Maoni

0 Maoni