Mwalimu wa Shule ya Sekondari Naputa Wilaya ya Tandahimba
mkoani Mtwara amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kuruhusu
kuingiliwa kinyume na maumbile.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mtwara, Issa Suleiman amesema
mwalimu huyo alijenga urafiki na mwanafunzi wa kidato cha nne kwa kuanza
kumnunulia vitafunwa shuleni na kumtaka akamtembelee nyumbani.
Amesema mwanafunzi huyo alipoenda nyumbani kwa mwalimu
alianza kumuonyesha video chafu kupitia simu janja na baadaye kumtaka
amuingilie kinyume na maumbile na alopokataa,mwalimu alianza kumtishia
Kamanda Suleiman amesema baada ya vitisho hivyo mwanafunzi huyo alilazimika kutekeleza kitendo hicho pasipo ridhaa yake.
0 Maoni