Rais na Mwenyekiti wa Bodi ya Simba, Mohammed Dewji amekutana
na kufanya mazungumzo na Simba Executive Network (SEN).
SEN ni mtandao wa mashabiki wa Simba ambao huchangia ada ya
1,500,000 kwa mwaka kwa ajili ya miradi maalumu ya miundombinu ya klabu.
Wanachama wa SEN hupata faida nyingi kama bima za maisha, tiketi za mechi na
faida nyingine nyingi.
Kikao hicho kilihudhuriwa na Viongozi wa SEN akiwapo
Mwenyekiti Abdulrazak Badru, Makamu wake Farouk Baghoza, Katibu Dkt. George
Ruhago, Katibu Msaidizi Richard Mwalibwa na wanachama wa SEN. Menejimenti ya
Simba iliongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu, Imani Kajula.
Malengo ya Mwaka: SEN inalenga kutengeneza uwanja wa mazoezi ili kuongeza idadi ya viwanja vya mazoezi Bunju.
0 Maoni