Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Dereva wa Sacania namba T979CVV na tela namna T758 BEU, Ross Mwaikambo (40), kwa kusababisha ajali iliyoua watu 13 katika eneo la Mbembela, Kata ya Iyunga Jijini Mbeya katika barabara kuu ya Mbeya- Tunduma.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya SACP Benjamin Kuzaga, amesema dereva huyo ambaye anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya akiwa chini ya ulinzi, alikuwa akitokea eneo la Shamwengo akiwa amepakia kokoto.
Amesema kwamba dereva huyo, aliligongana na gari namba T.167 DLF Toyota Coaster iliyokuwa ikiendeshwa na dereva asiyefahamika kisha kugongana na Gari namba T.120 DER Toyota Harrier iliyokuwa ikiendeshwa na Dokta Robert Francis Mtungi (48) Mkazi wa Isyesye.
Aidha, Lori hilo liliendelea kugonga Guta namba MC 660 BCR iliyokuwa ikiendeshwa na dereva asiyefahamika kisha kugonga Pikipiki namba MC 889 CKX iliyokuwa ikiendeshwa na dereva asiyefahamika na kusababisha vifo vya watu kumi na tatu (13) kati yao wanawake 5, wanaume 8 na majeruhi kumi na nane [18] kati yao wanawake 4 na wanaume 14 na uharibifu wa vyombo vya moto.
Kamanda Kuziga amesema majeruhi wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya kwa matibabu na miIli ya marehemu imepelekwa Hospitalini hapo kwa hifadhi na kusubiri k utambuliwa, huku akieleza kwamba chanzo cha ajali ni uzembe wa Dereva wa Gari namba T979CVV/T758 BEU kushindwa kulimudu gari kwenye mteremko.
0 Maoni