Ifanyeni Sekta ya uvuvi Afrika kuchangia Pato la Taifa- Dkt. Biteko

  

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka wadau wa sekta ya uvuvi  barani Afrika  kuhakikisha wanaifanyia kazi sekta ya uvuvi ili kuhakikisha inachangia kwenye pato la Taifa kwa kuhakikisha rasilimalizi za uvuvi zinalindwa.

Dkt. Biteko ameyasema hayo jana Mei 5, 2024 jijini Dar es Salaam wakati akifungua Mkutano wa Kwanza wa Wavuvi kufanyika baranı Afrika sambamba na Maadhimisho ya miaka 10 ya mafanikio ya sekta ya uvuvi wenye lengo la kutathmini sekta ya uvuvi ilipotoka, ilipo sasa na inapoelekea na kushirikisha  wadau mbalimbali,taasisi zinazowasaidia wavuvi wadogo zilizoko Afrika na kwingineko duniani.

“Nitoe wito kwenu wadau wa sekta ya uvuvi nchini kuhakikisha mnawapa kipaumbele wavuvi wadogo kwani ndio wanaochangia takribani asilimia 95 ya uvuvi wote Tanzania,” amesema  Dkt.Biteko

Ameongeza “Takwimu zinaonesha kuwa nchi Tanzania  inazalisha wastani wa tanı 475,579 za  samaki katı ya hızo tani 429,168 zinatokana na uvuvi katika maji ya asılı na kuchangia kiasi cha shilingi trilioni 3.4 ambapo ni karibu  na asilimia1.9 kwa mwaka.”

Aidha,  Dkt. Biteko amesema licha ya jitihada zinazochukuliwa kwenye sekta ya uvuvi Tanzania Kama ilivyo kwa  bara la Afrika bado inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo athari za mabadiliko ya tabianchi,ushirikishwaji mdogo wa wadau katika usimamizi wa shughuli za uvuvi hususani wanawake na vijana pamoja na upotevu wa mazao ya uvuvi baada ya kuvunwa.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema kuwa ni heshima kwa Tanzania kuwa mwenyeji wa Mkutano huo wa kwanza Afrika wa Wavuvi Wadogo ambao chimbulo lake ni Mkutano wa kuadhimisha Mwaka wa Kimataifa wa Wavuvi Wadogo na Wafugaji Viumbe kwenye Maji (IYAFA) uliofanyika Rome nchini Italia Machi, 2023.

Ameongeza kuwq lengo la Mkutano huo wa Kwanza wa Wavuvi Wadogo Afrika ni kutoa fursa kwa Wavuvi Wadogo kushiriki na kupaza sauti zao juu ya kuboresha uvuvi mdogo ikiwa ni pamoja na kuwezesha ushirikishwaji wa wavuvi wadogo kwenye michakato ya uundwaji na utekelezaji wa sera, sheria, kanuni, mipango na mikakati yote inayohusu wavuvi wadogo.  

“Ni muhimu kusema kwamba uchaguzi wa Tanzania haukuwa kwa bahati, ila ni kwa kutambua umuhimu wa uvuvi mdogo kwenye nchi yetu, na hatua ambazo nchi imechukua katika kuandaa na kutekeleza Mpango wa Nchi wa Utekelezaji wa Mwongozo wa Hiyari wa Uvuvi Mdogo”, amesema Mhe Ulega.

Amefafanua kuwa Kauli mbiu ya Mkutano huo “Muongo mmoja wa Maendeleo: Kuongelea baadaye ya Uvuvi Mdogo Endelevu” ilichaguliwa kutokana na kusherekea miaka kumi ya utekelezaji wa Mwongozo wa Hiyari wa  Uvuvi Mdogo ili kufikia uvuvi mdogo endelevu. Mkutano huu utafanya tathmini ya hali halisi ya utekelezaji Mwongozo huo wa hiyari, sambamba na utekelezaji wa muundo wa kisera na Mkakati wa Mageuzi ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji Afrika.

 “Tanzania ilikuwa nchi ya kwanza Duniani kuandaa Mpango kazi wa kutekeleza Mwongozo wa Hiyari wa wavuvi wadogo ambapo katika mkutano huu tutapata fursa ya kueleza uzoefu wetu kwa nchi nyingine,” amesisitiza Mhe. Ulega.



Chapisha Maoni

0 Maoni