Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbas
ameendesha Kikao Maalum cha Kamati ya Uongozi Mradi wa Kuboresha Usimamizi wa
Maliasili na Kukuza Utalii (REGROW) kwa lengo la kupata uwelewa wa pamoja juu
ya hatua mbalimbali zilizofikiwa za utekelezaji wa mradi kwa mwaka 2023/2024 na
hatua za utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2024/2025.
Katika kikao hicho Dkt. Abbas licha ya kupongeza jitihada
mbalimbali zilifanywa katika utekelezaji wa mradi, ameagiza Taasisi zote
zinazotekeleza Mradi kusimamia kikamilifu kazi zinazoendelea hususani Ujenzi wa
miundombinu ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati na si vinginevyo.
Dkt. Abbas amesisitiza kuwa, utekelezaji wa mradi wa REGROW
ni mkakati madhubuti wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan wa kuwaletea maendeleo
wananchi kupitia sekta ya utalii, hivyo utekelezaji wake ni lazima uwendane na
kasi ya Mhe. Rais Samia ya kuwainua wananchi kiuchumi.
Kikao hicho kikichofanyika Jijini Dodoma, kimeudhuriwa na wajumbe kutoka Wizara ya Maji, Wizara Kilimo, Wizara ya Fedha, Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Wizara ya Maliasili ambaye ndio inatekeleza mradi huo.
Na Sixmund Begashe
0 Maoni