Dk. Nchimbi akunwa na manufaa ya ushirikiano wa CCM na CPC

 

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. Emmanuel Nchimbi, ameelezea umuhimu wa ushirikiano unaovinufaisha vyama vya CCM na Chama cha Kikomonisti cha China (CPC) katika kikao chake na Mjumbe wa CPC Komredi Tang Degjie kilichofanyika Makao Makuu ya CCM Dar es Salaam.

Dk. Nchimbi ameelezea kuwa urafiki wa muda mrefu uliopo baina ya Tanzania na China, ulioimarika chini ya uongozi wa vyama vya CCM na CPC, umeendelea kudumu kwa zaidi ya miongo sita ya uhusiano wa kidiplomasia.

"Ushirikiano wa vyama vyetu hivi viwili ulianzishwa na waasisi wa mataifa yetu, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Mwenyekiti Mao Zedong, na tangu hapo umekuwa na kujikita katika ushirikiano wa kimkakati,” alisema Dkt. Nchimbi.

Dk. Nchimbi ameangazia mafanikio ya ushirikiano huo katika sekta ya ujenzi, afya, utalii, kilimo, madawa, biashara na uchumi, na kuhimiza China kuiunga mkono Tanzania kwa kuwekeza katika sekta zinazoanza kukua.



Chapisha Maoni

0 Maoni