Zoezi la kuwaondoa tembo kwenye
maeneo ya wananchi na kuwarejesha hifadhini kwa kutumia helikopta limeanza
katika Wilaya ya Mbarali, jumla ya makundi matano (5) yenye tembo 43
yameondolewa kwenye maeneo ya wananchi katika Kata ya Igava na kurejeshwa
Hifadhi ya Taifa Ruaha.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori
Tanzania (TAWIRI) Dkt. Eblate Ernest Mjingo amesema jana kuwa Wizara ya Maliasili na
Utalii imejipanga kuhakikisha changamoto hiyo ya uvamizi wa tembo inatatuliwa
ambapo timu ya wataalamu kutoka TAWIRI, TANAPA na TAWA ipo uwandani kuratibu
zoezi hili.
Dkt. Mjingo amesema zoezi hilo litaendelea kwa siku ya leo Mei 9, 2024 katika Kata nyingine za Wilaya ya Mbarali.
0 Maoni