Rais Samia apewa maua yake, ukuzaji wa utalii kwenye Mei Mosi

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kazi kubwa ya kutangaza utalii wa Tanzania duniani katika kilele cha maadhimisho  ya siku ya Mei Mosi 2024 jijini Arusha.

Pongezi hizo zimetolewa leo, Mei 01, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe Paul Makonda wakati akitoa salamu za mkoa wa Arusha.

Aidha, amesema tayari Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii na Wizara ya Mipango na Uwekezaji wanakusudia kujenga kituo cha Uwekezaji ambacho kitakuwa kikitoa huduma zote za sekt hiyo kwa Watalii na wawekezaji wa sekta ya utalii.

"Ndugu mgeni rasmi naomba niseme, jana tumefanya kongamano la Uwekezaji ha Arusha ambapo tumekubaliana kujenga One Stop Center kwa ajili ya kutoa huduma zote za utalii mahali pamoja." Amefafanua, Mhe. Makonda

Kongamano hilo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo, Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki (Mb),Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Dunstan Kitandula, Katibu Mkuu Maliasili Dkt. Hassan Abbasi, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Mbaga Kida, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda, Viongozi Waandamizi wa Chama na Serikali pamoja na Wadau wa Uhifadhi na Utalii wa jijini Arusha ambapo Mhe Kitila Mkumbo,  Waziri mwenye dhamana ya Mipango na Uwekezaji alikuwa mgeni rasmi

Aidha,  Watumishi wa Wizara ya  Maliasili na Utalii leo Mei Mosi 2024 wameungana na Wafanyakazi Duniani kote kuadhimisha  Siku hiyo hapa  nchini Tanzania mkoani Dodoma na kwenye Kilele cha Siku hiyo  kitaifa Jijini Arusha na Mgeni Rasmi wa Sherehe hizo ni Makamu wa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango

Wizara ya Maliasili imefanikiwa kutangaza vivutio vya utalii kupitia mashindano ya  michezo ya Mei Mosi 2024 yaliyoanza takribani  wiki tatu Iliyopita jijini Arusha na kufanikiwa  kunyakua vikombe mbalimbali.

Kauli mbiu ya siku hii ya Wafanyakazi Duniani kwa mwaka huu ni "Nyongeza ya Mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na kinga Dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha."

Chapisha Maoni

0 Maoni