Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), imepata
tuzo katika kipengele cha taasisi bora ya Serikali kidigitali ikiwa ni kutambua
mchango bora katika mageuzi ya kidigitali nchini Tanzania.
Tuzo hizo zimeandaliwa chini ya programu iitwayo Funguo
Innovation inayosimamiwa na UNDP kwa kushirikiana na Kampuni ya Serengeti Bytes
na Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH) yenye lengo la kutambua
michango mbalimbali inayotolewa na Taasisi za Serikali na Sekta Binafsi nchini
katika utoaji wa huduma kwa jamii.
Tuzo za Kidigitali kwa mwaka 2024 zilienda sambamba na maadhimisho ya miaka 10 ya wiki ya ubunifu ikiangazia mafanikio na changamoto katika ubunifu wa kidigitali.
0 Maoni