Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania-TFS umeshiriki na
kufadhili mkutano wa kitaaluma wa Wahariri wa Vyombo vya Habari nchini
uliolenga kuhamasisha uandishi wa habari katika matumizi ya gesi ili kulinda
misitu.
Akifungua mkutano huo Jijini Dodoma jana Aprili 29, 2024,
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Serikali
itahakikisha matumizi ya gesi yanapewa kipaumbele na kufanya jitihada ili
kupunguza gharama za mitungi ya gesi.
"Ifikapo mwaka 2034 tunataka asilimia 80 ya Watanzania
wawe wanatumia nishati safi ya kupikia" Dkt. Biteko.
Nae Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Meneja Sehemu ya
Baiolojia Mbegu za Miti Fandey Mashimba, akitoa wasilisho kuhusu kazi za TFS,
ameomba ushirikiano wa wahariri katika kufikisha elimu kwa umma na namna ya
kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya misitu na nyuki.
TFS ilipewa Cheti cha ufadhili kilichopokelewa na Meneja Uhusiano, Johary Kachwamba kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi-TFS, Prof. Dos Santos Silayo.
0 Maoni