Ramadhani Brother’s waanza kupanda Mlima Kilimanjaro

 

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Angela Nyaki, Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro amewaaga  vijana wa kitanzania almaarufu Ramadhani Brother’s jana tarehe 29.04.2024 kuianza safari ya ndoto yao ya kuelekea katika kilele kirefu kuliko vyote Barani Afrika cha Mlima Kilimanjaro chenye urefu wa mita 5,895 kutoka usawa wa bahari, safari inayotarajiwa kuchukua takribani siku 5 kupitia lango la Marangu.

Akiwaaga vijana hao waliojizolea umaarufu duniani kutokana na sanaa yao ya Sarakasi, Kamishna Nyaki alisema, "Lengo la Ramadhan Brother's kupanda mlima huu kwanza ni kuufahamu vizuri ili wanapouelezea kimataifa wasiwe na chembe ya mashaka, lakini pia kutangaza vivutio vingine vya utalii vinavyopatikana Tanzania watakavyotembelea baada ya kushuka mlima huu."

Pamoja na hayo Ramadhani Brother’s wamejikita katika kuhamasisha kampeni maalumu ijulikanayo kama “Vote Now” mahususi kwa ajili ya kupigia Kura Mlima Kilimanjaro na Serengeti zinazowania tuzo za World Travel Awards.

Chapisha Maoni

0 Maoni