Watu 15 wamepoteza maisha katika kipindi cha siku saba
kutokana na kusombwa na maji kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo
mbalimbali ya nchi.
Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini David Misime amesema
miongoni mwa watu hao, 12 walikuwa ni watoto na watu wazima ni watatu.
Misime amesema vifo hivyo vimetokea kati ya Aprili Mosi hadi
Aprili 07, 2024 katika mikoa ya Rukwa, Tanga, Geita, Pwani na Mbeya ambapo
baadhi ya vifo vya watu hao vilitokana na kusombwa na maji wakati wakiogelea na wengine
kusababishwa na mafuriko.
Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi limewaomba viongozi wa dini na taasisi
zingine kusaidia kutoa elimu kwa watanzania na uwekaji wa alama katika maeneo
hatarishi.
0 Maoni