Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii
inatarajiwa kesho tarehe 22.04. 2024 kutangaza rasmi matokeo ya sensa ya
wanyamapori, pamoja na kuzindua ripoti ya Watalii wa Kimataifa walioitembelea
nchini kwa mwaka 2023.
Utangazaji na uzinduzi huu huo utajumuisha wadau mbalimbali
wa uhifadhi na utalii utafanyika katika Hoteli ya Gran Melia Jijini Arusha,
ambapo Waziri wa maliasili na utalii Angellah Kairuki ndiye anayetarajiwa
kutangaza matokeo hayo ya sensa na kuzindua ripoti hiyo.
Katika mkutano wake na wanahabari jijini Arusha, Mwakilishi wa Wizara ya
Maliasili na Utalii
Dkt. Edward Kohi ambaye ni Mkurugenzi wa Utafiti
na Mafunzo amesema taarifa hizo
zenye tija katika uhifadhi wa
wanyamapori na kukuza utalii nchini zinaakisi juhudi za Serekali kuhifadhi
utajiri wa Maliasili ya
Wanyamapori na kukuza utalii nchini.
Aidha, ripoti hiyo itaangazia matokeo watalii walioitembelea nchi hii mwaka 2023 baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia filamu ya Royal Tour.
0 Maoni