Mchezaji wa Brazil aliyewahi kuichezea Manchester City na
Real Madrid, Robinho analazimika kutumikia kifungo cha miaka tisa jela kwa
ubakaji nchini Brazil.
Robinho, 40, alitiwa hatiani na Mahakama ya Italia mwaka 2017
kwa kushiriki na wenzake kumbaka mwanamke mwenye miaka 22 raia wa Abainia.
Hapo jana, Majaji katika Jiji la Brasilia walisema kuwa
Robinho anapaswa kutumikia kifungo hicho nchini Brazil, kufuatia maombi ya
Italia.
Hata hivyo, Robinho ataendelea kuwa huru kufuatia rufaa aliyoikata
dhidi ya hukumu hiyo, Wakili wake amesema.
Mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Brazil, aliyelichezea
taifa lake michezo 100, wakati wa tukio hilo alikuwa anaichezea AC Milan.
Baada ya kutia hatiani alishindwa rufaa yake mwaka 2020, na kisha
Mahakama ya Juu ya Italia ikakazia hukumu yake mwaka 2022.
Baada ya kushindwa rufaa waendesha mashataka wa Italia,
walitoa hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa Robinho.
Robinho, ambaye aliichezea Manchester City kwa muda wa miaka
miwili, Jumapili alikiambia chomba cha habari cha Brazil kwamba kulikuwa na
makubaliano ya kufanya ngono.

0 Maoni