TAWA yafanya makubwa miaka mitatu ya Rais Samia

 

Mamlaka ya Uhifadhi na Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), imefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi bilioni 184.74 katika kipindi cha kati ya mwaka 2020/21 hadi 2024.

Hayo yamesemwa na Kamisha wa Uhifadhi na Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Kamishna Mabula Misungwi Nyanda, Jijini Dar Es Salaam Machi 18, 2024, wakati akitoa wasilisho la mafanikio ya TAWA kwa kipindi cha miaka mitatu (2021/22-2023/24 ) ya serikali ya awamu ya sita ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amesema juhudi za makusudi zilizofanywa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutangaza utalii kupitia filamu ya Royal Tour, Fedha za UVIKO 19 chini ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19 (Tanzania Social Economic Response and Recovery Plan (TCRP ) ambapo TAWA imefaidika kwa kuimarisha miundombinu wezeshi ya Utalii katika maeneo mbalimbali.

Ametaja maeneo hayo ni pamoja na ujenzi wa Kilomita 431.4 za barabara katika Mapori ya Wamimbiki, Mpanga Kipengere, Igombe, Swagaswaga, Mkungunero, Kijereshi, Rungwa na Pande,

Aidha, TAWA pia imeweza kukarabati viwanja vya ndege vitatu (3) katika Pori Tengefu Lake Natron (Engaresero) na Pori la Akiba Maswa (Buturi na Mbono),

Pia, kujenga miundombinu ya kupumzika wageni (Bandas 13, Campsites - 6, picnic sites - 8, lounge 1) na hostel 1 katika Mapori ya Akiba Mpanga Kipengere, Mkungunero, Lukwika Lumesule, Pande Swagaswaga na Magofu ya Kilwa.

Kamishna Nyanda pia amesema, mafanikio mengine ni pamoja na ujenzi wa malango matano (5) na vituo vinne (4) vya kukusanyia mapato katika Mapori ya Akiba ya Wamimbiki, Mkungunero, Lukwika Lumesule, Swagaswaga, Mpanga Kipengere, Kijereshi na katika Pori Tengefu Ziwa Natron,

Ujenzi wa njia ya waenda kwa miguu zenye urefu wa kilometa 3.7 katika Pori Tengefu Ziwa Natron, na Mapori ya Akiba Swagaswaga, Kilwa Kisiwani na Mpanga Kipengere,

Miundombinu mingine iliyoimariswa ni ukarabati wa mabanda sita (6) ya Utalii katika Pori la Akiba Wamimbiki.

Aidha, Kamishna Nyanda amesema kumekuwepo na ongezeko la Wawindaji kutoka 355 mwaka 2020/21 hadi wawindaji 787 mwaka 2022/23 na wawindaji 481 hadi Februari mwaka 2024, lakini pia kuongezeka kwa idadi za meli za Kimataifa za utalii kutembelea eneo la Kihistoria Kilwa.

Chapisha Maoni

0 Maoni