Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Hussein Ali Mwinyi amepokea salamu za pole Ikulu Mnazi Mmoja kutoka kwa Luteni
Jenerali Mstaafu Samuel Ndomba ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la
Mzinga kwa niaba ya uongozi wa shirika hilo, kufuatia kifo cha Baba
yake Mzazi, Rais Mstaafu wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati
Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Rais Dk. Mwinyi ameshukuru uongozi wa shirika hilo kwa kuja
kumfariji.
Pia, Rais Dk. Mwinyi amepokea pole kutoka kwa Mh. Makamba
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Hussein Ali Mwinyi amepokea salamu za pole Ikulu Mnazi Mmoja kutoka kwa Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba kufuatia
kifo cha Baba yake Mzazi, Rais Mstaafu wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Pia katika mazungumzo yao wamegusia shughuli za uendeshaji wa ofisi ya Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar.
0 Maoni