Uongozi wa NHIF ukiongozwa na Mkurugenzi wa Huduma za
Matibabu Dkt. David Mwenesano wametembelea na kukutana na uongozi wa Hospitali
ya Bochi baada ya Hospitali hiyo kuandika barua ya utayari wa kuanza kuhudumia
wanachama wa NHIF.
Hospitali iliyopo Jijini Dar es Salaam tayari imesaini mkataba
kwa ajili ya utekelezaji wa kitita kipya na huduma zimerejea kama kawaida kwa
wanachama wa NHIF.
Hapo jana hospitali kadhaa za binafsi ziliandika notisi ya
kusitisha kutoa huduma kwa wanachama wa NHIF, wakisusia kitita kipya cha huduma
za NHIF.
0 Maoni