Kazi ya Marekebisho ya Pampu ya kusukuma maji katika mtambo wa kuzalisha maji Ruvu Chini sasa imekamilika rasmi.
Marekebisho haya yaliyopelekea upungufu wa uzalishaji maji
kutoka lita milioni 270 hadi lita milioni 220 kwa siku, na kusababisha uhaba wa
maji katika maeneo mengi ya Dar es Salaam.
Matengenezo yamekamilika leo, Februari 26, 2024 na kurudisha
hali ya uzalishaji katika kawaida yake ya ujazo wa lita milioni 270 kwa siku.
Taarifa iliyotolewa imesema kufuatia kazi hiyo kukamilika maeneo
yafuatayo yataanza kupata huduma ya maji kwa msukumo mzuri. Maeneo hayo ni kama
yafuatayo:-
Bagamoyo, Mapinga, Mabwepande, Bunju, Tegeta, Mbweni, Boko, Salasala, Goba, Mivumoni, Kawe, Lugalo, Makongo, Chuo, Kikuu, Mwenge, Kijitonyama, Mikocheni, Msasani, Oysterbay, Masaaki, Mwananyamala, Kinondoni, Magomeni, Kigogo, Chang'ombe, Keko, Kurasini, Kigamboni, Airport, Kiwalani, Buguruni, Vingunguti, Ilala na Katikati ya Jiji.
0 Maoni