Rais Dk. Mwinyi akutana na Jumuiya ya Mabunge ya Canada na Afrika

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amekutana na Balozi wa Canada nchini Tanzania, Kyle Nunas na ujumbe wa Wenyeviti wa Jumuiya ya Mabunge ya Canada na Afrika wakiongozwa na Seneta, Amina Gerba Ikulu Zanzibar tarehe:22 Februari 2024.

Rais Dk. Mwinyi amesema sekta kuu ya uchumi wa Zanzibar ni utalii ambao unachangia asilimia 30 ya pato la Taifa, pia ameikaribisha Canada kuangalia fursa zilizopo katika  uchumi wa buluu ikiwemo utalii, uvuvi, usafiri wa vyombo vya baharini, bandari , mafuta na gesi.

Halikadhalika Rais Dk. Mwinyi ameishukuru Serikali ya Canada kwa ushirikiano wa miradi mbalimbali ya huduma za kijamii ikiwemo elimu na afya.

Vilevile Rais Dk. Mwinyi amesema Muungano wa Tanzania ni wa kipekee utaendelea kuwa mfano wa kuigwa Afrika.

Pia katika mazungumzo hayo amegusia suala la uhuru wa habari, Serikali ya umoja wa kitaifa, nafasi za uwakilishi kwa Wanawake, uwekezaji pamoja na nishati hususani umeme.



Chapisha Maoni

0 Maoni