Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj
Dk. Hussein Ali Mwinyi amewahimiza malezi bora katika jamii ili kujiepusha na
vitendo viovu ikiwemo matumizi ya dawa za kulevya, wizi, ubadhirifu wa mali za
umma, udhalilishaji na ulevi.
Rais Dk. Mwinyi amesema malezi bora yanaanzia ngazi ya
familia, pia amewataka wazazi na walezi Kuwalea vijana katika malezi mema yenye
maadili.
Rais Dk. Mwinyi amesema hayo alipojumuika na Waumini wa Dini
ya Kiislamu katika ibada ya Sala ya Ijumaa Msikiti wa Makuti Kisiwandui Mkoa wa
Mjini Magharibi tarehe 16 Februari 2024.
Rais Dk. Mwinyi ameshiriki katika ibada ya sala ya Ijumaa Misikiti mbalimbali Unguja na Pemba mpaka sasa idadi yake ni 133 pia amefungua Misikiti mipya 28 Unguja na Pemba.
0 Maoni