Mwili wa Waziri Mkuu Mstaafu Edward Ngoyai Lowassa umewasili
leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), na kupokelewa na
viongozi mbalimbali waliofika uwanjani hapo.
Mwili wa Lowassa umewasili KIA leo Februari 15, 2024 majira
ya saa 5:22 asubuhi ukitokea Dar es Salaam na kupokelewa na waombolezaji waliwamo
wakuu wa mikoa, Nurdni Babu, John Mongela na Waziri Kindamba wakiwa na Kamati
ya Usalama.
Baada ya mwili wake kuwasili, msafara wa kwenda kijijini
kwake Ngarash, Wilayani Monduli mkoani Arusha ulianza ukiwa na magari zaidi ya
100 likiwemo la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lililoubebeba
mwili huo.
Lowassa aliyefariki dunia Februari 10, 2024 katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu, atazikwa jumamosi Februari 17, nyumbani kwao katika kijiji cha Ngarash.
0 Maoni