Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar, Simai Mohammed Said ameiteua timu ya Simba Sports Club kuwa Balozi
wa Utalii visiwani humo.
Hatua hii inafuatia klabu ya Simba kuonyesha dhamira ya
kutangaza utalii wa Zanzibar kupitia kauli mbiu ya Visit Zanzibar katika jezi zao
pamoja na mitandao ya kijamii wakati wa michuano ya Kombe la Mapinduzi.
Mtendaji Mkuu wa Simba Iman Kajula imeishukuru Serikali ya Mpinduzi ya Zanzibar kwa kutambua mchango wa Klabu ya Simba kwa kutangaza utalii Zanzibar pamoja na kusaidia kuipa hadhi ya Kimataifa michuano ya Kombe la Mapinduzi.
0 Maoni