Msemaji wa Simba SC Ahmed Ally amesema klabu hiyo imeamua
kuyabeba mashindano ya Mapinduzi Cup ili kuyapa thamani ambayo itaifanya kila
timu Afrika itamani kushiriki, ione raha kuja Zanzibar.
“Kuanzia mechi ya kesho dhidi ya Singida Fountain Gate
tutavaa jezi zenye nembo ya Zanzibar. Ndani ya siku hizi 14 za kuchukua ubingwa
wa Mapinduzi tutatembelea maeneo ambayo yana vivutio vizuri lakini havionekani
sana, sisi tutaitangaza kupitia kwenye kurasa zetu,” amesema Ally.
Lengo letu ni moja tu kuongeza namba ya watalii hapa visiwani Zanzibar. Nawaomba Wanasimba tukitangaza sehemu ambayo tunatembelea mjitokeze kwa wingi, amesema Ally. #UchumiWaBuluu #VisitZanzibar #WenyeNchi #NguvuMoja
0 Maoni