JUMLA ya ekari 100 kutoka Jeshi la Magereza kwenye eneo la
Warret, Wilayani Hanang zimetolewa kwa ajili ya waathirika.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Geophrey Pinda ametembelea na kukagua eneo hilo lililotolewa na Jeshi la
Magereza ambapo tayari eneo hilo limepimwa viwanja kwa ajili ya kuwahamisha
waathirika wa mafuriko yaliyotokana na maporomoko ya mawe na tope kutoka mlima
Hanang.
Pinda amefanya ukaguzi huo akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa
Manyara, Queen Sendiga pamoja na viongozi wengine wa mkoa pamoja na wa wilaya
ya Hanang.
Desemba 21, 2023 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Jenister Mhagama alielekeza Wizara ya Ardhi kuhakikisha viwanja kwa ajili ya kuhamisha waarhirika maeneo ya Gendavi, Jorodom, Ganana na Katesh - Hanang vinapimwa na kukamilika kabla ya Desemba 31, 2023.
0 Maoni