Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro amefanya mazungumzo maalumu na kikosi cha timu ya Taifa (Taifa Stars)
kilichoweka kambi katika Jiji la San Pedro nchini Ivory Coast kujiandaa na
mchezo wa kwanza wa mashindano ya AFCON 2023 dhidi ya Morocco.
Mhe. Ndumbaro amezungumza na wachezaji hao mara baada ya
kushuhudia mazoezi na utayari wa
kikosi hicho kuelekea mchezo wao na Timu
ya Taifa ya Morocco utakaopigwa jijini humo Januari 17, 2024.
Baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa muda wa takribani saa
mbili, Waziri Dkt. Damas Ndumbaro amesema ameridhishwa na maandalizi ya kikosi
hicho, Ari na morali ya wachezaji na benchi la ufundi ambayo inatoa picha nzuri
ya kufanya vizuri katika kundi F la michuano hiyo.
Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF), Bw. Wallace Karia, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) ambaye pia ni Mkuu wa msafara wa timu Bw. Suleiman Mahamoud Jabir.
Na, Brown Jonas-WUSM
0 Maoni