Mtumiaji youtube amehukumiwa miezi sita jela kwa kuangusha
ndege kwa makusudi ili kupata watazamaji wengi (views), na kuwadanganya
wachunguzi wa ajali wa Marekani.
Trevor Jacob, 30, aliiposti video ya ndege ikianguka Desemba
2021, akidai kuwa ni ajali, na kuruka kutoka kwenye ndege akijichukua picha za selfie
huku akishuka chini kwa parachuti
Video hiyo ya ajali ya kupangwa ilitazamwa mara nyingi na mamilioni
ya watu kwenye youtube channel yake.
Katika makubaliano ya kukiri kosa hilo, Jacob alisema kuwa alipiga
picha ya ajali hiyo ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya udhamini wa bidhaa.
0 Maoni