Cristiano Ronaldo amefikisha magoli 1,200 katika mechi
zinazotambulika rasmi kimataifa kwenye mchezo wa soka baada ya kufunga goli
moja na kusaidia jingine moja kwa timu yake ya Al-Nassr.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 38, aliunganisha ndani ya
nyavu mpira wa krosi uliopigwa na Sadio Mane, na baadae akamtengenezea goli Otavio
katika ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Al-Riyadh.
Ronaldo alitumia ushindi huo kuwashukuru wale wote
waliomsaidia katika kufikisha rekodi hiyo, na kuongeza kwa kusema kuwa bado
hajamaliza.
Mshambuliaji huyo raia wa Ureno anaongoza kwa ufungaji
katika Ligi ya Saudi, akiwa ametikisa nyavu mara 16 katika mechi 15 kwenye msimu
huu.
0 Maoni