Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amewataka watendaji wa kata na mitaa kuwa waadilifu wakati wote wanapotekeleza majukumu yao kwa kuwa wanaishi na jamii moja kwa moja vile vile miradi mingi ya mendeleo inatekelelezwa katika ngazi ya Kata au mtaa
RC Chalamila ameyasema jana
wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya maafisa Tarafa na watendaji wa kata wa mkoa wa
Dar es salaam uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke
yatakayofanyika kwa siku mbili kuanzia jana hadi leo Novemba 24,2023.
Vilevile amesema watumishi
wanapaswa kuwa na maadili ili kuleta picha nzuri kwa wananchi ikiwa
wakiharibu lawama za wananchi zinaenda moja kwa moja kwa viongozi wa juu.
Aidha, Mhe. Chalamila
amewataka watumishi hao waelewe uadilifu si umaskini na utajiri si wizi,
"Kuna utofauti mkubwa kati ya uadilifu na umaskini na wengi wanadhani
muadilifu ni kuwa maskini, kwahiyo acheni kuishi kimaskini ili muonekane ni
waadilifu."
Pia RC Chalamila amesema
mafunzo hayo yana umuhimu mkubwa sana na aliwaasa viongozi hao kutatua kero na
changamoto za wananchi ikiwemo migogoro ya ardhi, kusimamia amani na usalama
wao, usimamizi mzuri wa miradi na pesa wanazokabidhiwa zitumike kama
zilivyopangiwa, wajiepushe na vitendo vya rushwa na kuwadhulumu wanyonge haki
zao.
Naye Mkuu wa wilaya ya
Temeke Mhe Sixtus Mapunda alisema mafunzo ni mama wa uelewa wa mambo yote na
kuhimiza yawe yanatolewa mara kwa mara ili kuzidi kuwajengea uwezo na kutambua
nafasi zao kama watumishi sababu wao ndiyo wapo karibu zaidi na wananchi na
kutambua kero na changamoto zao.
Kwa upande wa mwenyekiti wa
mafunzo hayo Hulda J. Ulomi alitoa neno la shukrani kwa Mhe Chalamila kwa
kufunguzi na maelezo yake, na kuahidi kwamba watafuatilia mafunzo yote kwa
umakini na kwenda kuwa bora zaidi katika utendaji wa majukumu yao.
0 Maoni